Leteipa The King – Ndoto ya mchana lyrics

Album: Teipa tales

Intro:
Iyeeeh iyeeh iyeeeh, Ni vampK
lalalalalala lalalalalaaaa
Verse 1
Niliskia tufununu, Kwamba ulipata mwingine,
Anayekupenda zaidi ya mimi, mtafunga ndoa pengine,
Yetu ilikuwa shadow, mapenzi yenu yamekolea,
Lazima huwa Anakupa, vitu sikuwa nakupea,
Ndoto zako zote, ulizoniambia,
Naona kama kweli sasa zinatimia,
Na Sina chochote, cha kukuambia,
Ila nakonda Kweli nikikufikiria,

Hook:
Sura yako umbo lako jamani eeh,
Busu na mahaba chumbani maami ,
Mawaidha yako nikiwa matatani eeh,
Nikikumbuka najiona hayawani maami

Chorus:
Nawatakia mema, (Nawatakia mema)
#ss$## mema, (Nawatakia mema)
Nawatakia mema, (Nawatakia mema)
Basi kwaheri kwaheri kwaheri Mami (Ndoto yangu ya Mchana)

Verse 2:
Ingawa inaniuma, niko na furaha moyoni,
Kuona kwamba umepata, vyote ulivyokuwa unatamani,
Naomba nipate mwaliko, wa harusi nije Nile wali,
Nipige picha na wadau, nikupe zawadi kama zamani
Alafu ntapeform, kama beshte yako, kale kawimbo nilikuimbia shambani
Na nitakuinform, tunza mume wako, Japo kuna vitu zenye ninatamani,

Hook:
Sura yako umbo lako jamani eeh,
Busu na mahaba chumbani maami ,
Mawaidha yako nikiwa matatani eeh,
Nikikumbuka najiona hayawani maami

Chorus:
Ingawa ningependa,ungekuwa wangu pekee, (Nawatakia mema)
Ingawa moyoni umeniachia kidonda, (Nawatakia mema)
Namwomba Mungu, anipatie mwingine Kama wewe, (Nawatakia mema)
Hivo kwaheri kwaheri kwaheri kwaheri mama (Ndoto yangu ya Mchana)
Lakini ninaomba, unifanyie favour Moja (Nawatakia mema)
Ukijifungua kama ni wa kiume,mpe jina laangu (Nawatakia mema)
Na kama ni wa kike mpe jina la mama yangu (Nawatakia mema)
Basi kwaheriiiiiiii (Ndoto yangu ya Mchana)

Submitted by Guest